Sunday 9 July 2017

Magazeti Jumapili July 9, 2017

































Share:

Saturday 28 January 2017

Vijana wawili waweka rekodi kwa kufunga ndoa rahisi isiyokuwa na mbwembwe.

Wanaume wengi tunapenda kufunga ndoa za gharama nafuu lakini wenza wetu ukiwapa mkakati huo wanageuka mbogo na kuwa wachungu kama shubili. Sasa ebu tuchukue somo kupitia vijana hawa kutoka nchini Kenya.

Vijana wawili wapenzi ambao stori yao kuhusu ndoa ya bei rahisi waliyofunga ilizua hisia za watu wengi kwenye mitandao ya kijamii, sasa wameahidiwa kulipiwa gharama zote za mapumziko baanda ya ndoa (honeymoon).


MUTURA3-750x375.jpg

Wilson Mutara (26) na Ann Wambui (24) kutoka nchini Kenya inaripotiwa kuwa walifunga ndoa kwa gharama ya Ksh 100 ambayo ni sawa na TZS 2,147 ambapo gharama hizo zilikuwa kwa ajili ya kununua pete tu.


C3J9guVVUAAGPN0.jpg

Ndoa hiyo iliyotajwa kuwa ya bei rahisi kuwahi kutokea nchini humo haikua na sherehe baada ya wawili hao kutoka kanisani na walivalia fulana walipokwenda kufunga ndoa.

“Tulikwenda nyumbani tukapika ugali na sukuma wiki, tukala na tukalala. Hakuna kitu cha kipekee tulichokifanya katika mapumziko (honeymoon) yetu” alisema Mutura.

C3J9gzGUkAEys3K.jpg
Mchungaji aliyefungisha ndoa hiyo alichapisha habari hiyo na ndipo mwakilishi wa Kampuni ya Utalii ya Bonfire Adventure alipokutana na wanandoa hao.

C3MA8bzWIAAwt5I.jpg

Kampuni hiyo ndiyo ilijitolea kudhamini mapumziko ya wawili hao baada ya kufunga ndoa.
Share:

Thursday 20 October 2016

Polisi yauwa majambazi Dar


WATU sita wanaotuhumiwa kuwa majambazi hatari, wameuawa katika majibizano ya risasi na Polisi katika eneo la Mbezi kwa Yusuf Makondeni katika Manispaa ya Kinondoni, Dar es Salaam.
Kwa mujibu wa Kaimu Kamanda wa Kanda Maalumu, Naibu Kamishna wa Polisi, Lucas Mkondya, watuhumiwa hao waliuawa katika majibizano ya risasi na Kikosi Maalumu cha Kupambana na Ujambazi wa Kutumia Silaha.
Mkondya alisema wamepata taarifa kutoka kwa raia mwema kuwa kuna kikundi cha watu wenye silaha, wamejipanga kufanya tukio la ujambazi kwa kutumia silaha kwa mfanyabiashara aliyekuwa akitoka Benki ya Diamond Trust Bank (DTB), tawi la Barabara ya Nyerere, ambaye angepita katika barabara hiyo kwenda mkoani Morogoro.
Alisema baada ya kupata taarifa hizo, polisi waliweka mtego na majambazi hao wakitumia gari aina ya Toyota Carina lenye namba za usajili T970 DGZ rangi ya fedha, walionekana wakilifukuza gari la mfanyabiashara huyo, kisha kulipita na kumsimamisha kwa nguvu.
“Majambazi wawili wakiwa na bastola walishuka katika gari hilo. Baada ya kugundua kuwa wameingia kwenye mtego wa polisi, walianza kufyatua risasi kwa askari wakitumia bastola na wenzao waliokuwa wamejaa kwenye gari yao walianza kushuka huku wakifyatua risasi kuelekea kwa askari,” alisema Kaimu Kamanda Mkondya.
Alisema kutokana na hali hiyo, askari walianza kujibu mashambulizi na kuwaua majambazi hao na baada ya upekuzi, zilipatikana bastola mbili, moja ya kijeshi aina ya Chinese ikiwa na risasi moja ndani ya kasha la risasi; na nyingine aina ya Browning ikiwa imefutwa namba zake na maganda sita ya risasi yaliyookotwa katika eneo la tukio.
Miili ya watuhumiwa hao imehifadhiwa katika Hospitali ya Taifa Muhimbili (MNH) na upelelezi unaendelea ili kubaini mtandao mzima wa ujambazi.
Katika tukio lingine la Oktoba 17, mwaka huu saa 2:00 usiku katika maeneo ya Tegeta Masaiti, watuhumiwa watatu wa ujambazi wakiwa wamepakizana kwenye pikipiki aina ya Fekon yenye namba MC370 BEY, wakiwa na bunduki aina ya shotgun iliyokatwa mtutu na kitako, walivamia duka la Abdallah Juma (46), mkazi wa Tegeta na kupora fedha za mauzo na kuiba vocha za mitandao mbalimbali, ambazo thamani yake haijafahamika.
“Polisi baada ya kupata taarifa waliwafukuza majambazi hao, walipoona wanakaribiwa na askari, walitupa chini begi walilokuwa nalo na kutelekeza pikipiki yao kisha kukimbia, begi lilipopekuliwa lilipatikana na silaha hiyo,” alisema.
Aidha, wananchi wenye hasira waliendelea kuwakimbiza majambazi hao na kumuua mmoja huku wengine wakikimbilia kusikojulikana. Katika hatua nyingine, Mkondya alisema wamekamata watuhumiwa wawili wa unyang’anyi kwa kutumia nguvu wakiwa na pikipiki moja na funguo bandia 75.
Alisema watuhumiwa hao, Ally Makwega (53) mkazi wa Tandika na Fabian Greyson (39) mkazi wa Yombo walikamatwa Oktoba 4, mwaka huu saa 6:00 usiku.
Watuhumiwa hao walikamatwa wakiwa na pikipiki yenye namba MC292 AMD aina ya Boxer rangi nyekundu, wanayoitumia kufanya uhalifu, wakiwa na funguo bandia 75 ambazo huzitumia katika kuvunja nyumba mbalimbali ya biashara za kulala wageni, maghala ya kuhifadhia bidhaa na maduka.
Baada ya watuhumiwa hao kuhojiwa, walikiri kuhusika na matukio mbalimbali ya uvunjaji wa maghala na kuiba katika mikoa ya Dar es Salaam, Morogoro na Dodoma.
Watuhumiwa hao watafikishwa mahakamani baada ya upelelezi kukamilika. Mkoani Tanga, Anna Makange anaripoti kuwa mtoto wa kiume mwenye umri wa miaka mitano ambaye ni mkazi wa Kata ya Sindeni wilayani Handeni, ameuawa kwa risasi na mjomba wake mwenye umri wa miaka sita wakati walipokuwa wakichezea bunduki aina ya gobori nyumbani kwao.
Tukio hilo la kusikitisha, limetokea katika Kijiji cha Kweditilibe, wakati watoto hao ambao ni ndugu wa familia moja walipokuwa wakichezea bunduki hiyo inayomilikiwa na baba wa mtoto aliyeuawa.
Kamanda wa Polisi Mkoa wa Tanga, Benedict Wakulyamba alithibitisha jana kutokea kwa mauaji hayo na kusema yalifanyika Oktoba 17, mwaka huu saa 12:30 jioni.
“Siku hiyo ya tukio, mmiliki wa gobori hilo ambaye ndiye baba mzazi wa mtoto aliyeuawa, inadaiwa alikuwa ameliweka hapo nyumbani na ndipo hao watoto wakaingia na kulichukua kwa ajili ya kulitumia wakati wakicheza nje na ndipo mtoto ambaye inadaiwa ni mjomba wa marehemu alipomfyatulia risasi mwenzake na kusababisha kifo hicho,” alisema Kamanda Wakulyamba.
Kamanda Wakulyamba alisema mmiliki wa gobori hilo ambaye ni mzazi wa marehemu, anaendelea kutafutwa na polisi kwa kuwa hakuweza kupatikana baada ya mauaji hayo na kwamba uchunguzi kuhusu tukio hilo bado unaendelea.
Katika tukio jingine lililotokea kwenye Kata ya Mazinde wilayani Korogwe, mfugaji Maliki Kilimbo (18) amejeruhiwa kwenye goti lake la mguu wa kushoto kwa kupigwa risasi wakati akilisha mifugo ndani ya shamba la mwekezaji. Kamanda Wakulyamba alisema uhalifu huo ulifanyika Oktoba 17, mwaka huu saa 12:30 jioni wakati mfugaji huyo alipoingiza mifugo kwenye shamba la mkonge, mali ya Kampuni ya Toronto.
“Kilimbo alijeruhiwa kwa risasi ya bunduki aina ya gobori na mlinzi wa Kampuni ya Toronto aitwae Benjamin Mgiriki.... upelelezi kuhusu tukio hili bado unaendelea,” alisema.
Mkoani Rukwa, Peti Siyame anaripoti kuwa wananchi katika Kijiji cha Legezamwendo wilayani Sumbawanga, wamemuua kwa kumkata kata kwa mapanga mkazi wa kijiji cha Mkusi, Erick Nkrukizi (30) na kuuchoma moto mwili wake baada ya kumkamata akitaka kuumua mwanamke, Nkundi Masingija.
Kamanda wa Polisi Mkoa wa Rukwa, George Kyando alisema mauaji hayo yalifanyika Oktoba 19, mwaka huu, saa mbili usiku, baada ya kundi la watu hao, kufanya mauaji hayo. Watu hao hawajafahamika. Uchunguzi wa polisi unaendelea ili kuwabaini na kuwafikisha kwenye vyombo vya dola ili sheria ichukue mkondo wake.
Share:

Wednesday 19 October 2016

Waziri Mkuu aagiza wanaoharibu mazingira kuchukuliwa hatua


Waziri Mkuu KASSIM MAJALIWA ameuagiza uongozi wa mkoa wa LINDI kuhakikisha wanawakamata na kuwachukulia hatua za kisheria
Waziri Mkuu KASSIM MAJALIWA ameuagiza uongozi wa mkoa wa LINDI kuhakikisha wanawakamata na kuwachukulia hatua za kisheria watu wote wanaoharibu mazingira kwa kufyeka na kuchoma moto misitu. 
Waziri Mkuu MAJALIWA ametoa agizo hilo kwa nyakati tofauti wakati akizungumza na wananchi wa wilaya ya RUANGWA kwenye mikutano ya hadhara ambapo amesema mkoa huo uko hatarini kugeuka jangwa na tayari vyanzo vingi vya maji vimeanza kukauka kwa sababu ya uharibifu wa mazingira unaosababisha ukame.
Kwa upande wake Mkuu wa Mkoa wa LINDI, GODFREY ZAMBI, amewataka watendaji wa kata na vijiji kuimarisha ulinzi wa maeneo ya misitu na maji na atakayeshindwa atachukuliwa hatua kali za kisheria.
Wakati huo huo Mke wa Waziri Mkuu MARY MAJALIWA
ameiomba jamii ya watanzania kuwasaidia watoto wenye ulemavu wa ngozi.
Mama MAJALIWA ameyasema hayo wakati alipokwenda kutoa misaada kwa watoto wenye ulemavu huo katika kijiji cha MITOPE kilichopo wilaya ya RUANGWA Mkoani LINDI.
Share:

Viongozi wa Mila wa jamii ya Wamasai wametakiwa kusuluhisha na kutatua migogoro ya ardhi


Viongozi wa Mila wa jamii ya Wamasai wametakiwa kusuluhisha na kutatua migogoro ya ardhi,maeneo ya malisho pamoja na wizi wa mifugo ili kuepusha uvunjifu wa amani na kuzorota kwa maendeleo kunakosababishwa na migogoro hiyo.
Hayo yameelezwa na Wazee wa Mila Peter Toima na Lemamiye Shininii wakati wa sherehe za kuhama rika ambao Maelfu wa vijana kutoka Wilaya ya Simanjiro wanahamia rika la wazee na kukabidhiwa wajibu wa kuwa wasuluhishi katika jamii.
Wazee hao Walisema kuwa jukumu la kutatua migogoro linapaswa kufanywa na Wazee hao wapya na kuepuka kuitwisha serikali mzigo mkubwa wa migogoro ambayo wangeweza kuitatua .
Kwa upande wao Vijana waliohama rika na kuingia rika la wazee Oreka Mlolo na walisema kuwa kazi kubwa iliyoko mbele yao ni kuhakikisha kuwa jamii inaishi kwa amani ,kudumisha umoja na ushirikiano ambazo ni tunu muhimu kwa jamii ya Wamasai.
Mmoja wa Kinamama ambao Waume zao wameama rika Loema Thadey alisema kuwa mila hiyo hutumika kupima uaminifu wa Wanandoa iwapo Mwanamke anachepuka basi anaweza kupoteza maisha.
Jamii ya Wamasai ni jamii yenye tamaduni yenye nguvu iliyodumu kwa muda mrefu na kuenziwa licha ya changamoto ya utandawazi uliomeza tamaduni nyingi za Kiafrika na kuleta utamaduni wa nchi za Magharibi.
Share:

Wanaopata mikopo ya elimu ya juu ni wenye vigezo na uhitaji tu


Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia na mafunzo ya ufundi, imesema mikopo inayotolewa kwa wanafunzi wa elimu ya juu inatolewa kwa wahitaji kwa kuzingatia bajeti iliyopo.
Akizungumza jijini Dar es Salaam, naibu waziri, Bi Stella Manyanya amesema hali ya baadhi ya wanafunzi kukosa mikopo inatokana na wao kutokidhi vigezo.
“Tunaangalia wale wahitaji na uhitaji huo lazima uhakikishwe vizuri, kwasababu kuna watu wengine unakuta wanadiriki hata kusema uongo. Tumeshayashuhudia hayo sana. Mimi nina uhitaji wakati ana fahamu fika anataka tu fedha kwaajili ya kulewea pombe, anataka tu fedha kwaajili ya kutembelea,anataka anunue TV,mwingine anaamua kujenga sasa hivi akiwa shuleni, sasa hatuwezi kwenda katika sura hiyo,lazima tuthibitishe kwa kina,kwamba huyu kweli ni mtu mwenye uhitaji na mwenye uhitaji aweze kusaidiwa,bila kujali kwamba huyu yuko wapi,lakini tunaenda hatua kwa hatua,”alisema.
“Lakini ninaposema wenye uhitaji lazima tukubaliane kwamba kama sheria inavyosema kwamba pamoja na uhitaji si rahisi kwamba wote kabisa wakapata,lazima kuna wengine watajikuta wamekosa,lengo ni kwamba tumesaidia kwa kadri inavyowezekana, tumesaidia kwa jitihada zetu zote,”aliongeza.
Kwa upande wake mkurugenzi mtendaji wa bodi ya mikopo ya elimu ya juu, Abdurazak Badu, amesema awamu ya kwanza ya mikopo imeanza kutolewa kwa wanafunzi waliokidhi vigezo ambapo serikali imetoa shilingi bilioni 80 kwaajili ya mikopo hiyo huku serikali ikiwasisitiza wanafunzi hao kutumia mikopo hiyo kwa lengo lililokusudiwa.
Share:

Barcelona, Man City kukipiga leo


BARCELONA, HISPANIA
USIKU wa Ulaya unatarajia kuendelea leo kwa michezo nane kupigwa katika viwanja mbalimbali, huku mchezo unaotarajiwa kugusa hisia za watu wengi ni kati ya Barcelona ambao watakuwa kwenye uwanja wa nyumbani dhidi ya Manchester City.
Mbali na kuwepo kwa michezo mingi leo, dunia itasimama kwa muda kwa ajili ya kuutazama mchezo huu ambao ni wa kiufundi.
Makocha wa timu hizo wote waliwahi kuitumikia klabu ya Barcelona wakiwa kama wachezaji, lakini leo hii wanakutana na kuonesha ufundi wao, Pep Guardiola akiwa kocha wa Manchester City, huku Luis Enrique akiiongoza Barcelona.
Guardiola alikuwa na mchango mkubwa akiwa na klabu ya Barcelona tangu mwaka 2008 hadi 2012 alipojiunga na Bayern Munich ya nchini Ujerumani, aliipa mafanikio makubwa ambayo yatakumbukwa kwa kiasi kikubwa.
Katika mchezo uliopita wa klabu bingwa, Man City walikutana na Celtic na kutoka sare ya 3-3, leo hii wanakutana na Barcelona ambayo mchezo wao uliopita waliibuka na ushindi wa mabao 2-1 dhidi ya Monchengladbach.
Hata hivyo, Pep Guardiola ameshindwa kuzuia hisia zake kwa klabu ya Barcelona ambapo ameweka wazi kuwa mchezo huo utakuwa mgumu sana kutokana na ubora wa wapinzani wake.
“Najua uwezo wa klabu ya Barcelona, ninaamini mchezo utakuwa mgumu sana ubora wa wenzetu upo juu tofauti na sisi, lakini chochote kinaweza kutokea kwenye soka.
“Naweza kusema kuwa Barcelona ni kama mashine, kuna wachezaji watatu ambao ni hatari katika safu ya ushambuliaji,” alisema Guardiola.
Kwa upande wa Enrique, alisema hajazungumza na Guardiola, lakini anaamini mchezo huu utakuwa wa aina yake kwa kuwa Guardiola ana uwezo mkubwa.
Michezo mingine ambayo itapigwa leo ni pamoja na Napoli itakayopambana na Besiktas, Arsenal itacheza na Ludogorets, wakati huo FC Rostov wakipambana na Atletico Madrid, Dynamo Kyiv dhidi ya Benfica, PSG watacheza na FC Basel, Monchengladbach watacheza dhidi ya Celtic na Bayern Munich watacheza na PSV Eindhoven.
Share:

YouTube

Blog Archive

Pages

Our Facebook Page

Hali ya Hewa

Waliotembelea