Wednesday 19 October 2016

Wanaopata mikopo ya elimu ya juu ni wenye vigezo na uhitaji tu


Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia na mafunzo ya ufundi, imesema mikopo inayotolewa kwa wanafunzi wa elimu ya juu inatolewa kwa wahitaji kwa kuzingatia bajeti iliyopo.
Akizungumza jijini Dar es Salaam, naibu waziri, Bi Stella Manyanya amesema hali ya baadhi ya wanafunzi kukosa mikopo inatokana na wao kutokidhi vigezo.
“Tunaangalia wale wahitaji na uhitaji huo lazima uhakikishwe vizuri, kwasababu kuna watu wengine unakuta wanadiriki hata kusema uongo. Tumeshayashuhudia hayo sana. Mimi nina uhitaji wakati ana fahamu fika anataka tu fedha kwaajili ya kulewea pombe, anataka tu fedha kwaajili ya kutembelea,anataka anunue TV,mwingine anaamua kujenga sasa hivi akiwa shuleni, sasa hatuwezi kwenda katika sura hiyo,lazima tuthibitishe kwa kina,kwamba huyu kweli ni mtu mwenye uhitaji na mwenye uhitaji aweze kusaidiwa,bila kujali kwamba huyu yuko wapi,lakini tunaenda hatua kwa hatua,”alisema.
“Lakini ninaposema wenye uhitaji lazima tukubaliane kwamba kama sheria inavyosema kwamba pamoja na uhitaji si rahisi kwamba wote kabisa wakapata,lazima kuna wengine watajikuta wamekosa,lengo ni kwamba tumesaidia kwa kadri inavyowezekana, tumesaidia kwa jitihada zetu zote,”aliongeza.
Kwa upande wake mkurugenzi mtendaji wa bodi ya mikopo ya elimu ya juu, Abdurazak Badu, amesema awamu ya kwanza ya mikopo imeanza kutolewa kwa wanafunzi waliokidhi vigezo ambapo serikali imetoa shilingi bilioni 80 kwaajili ya mikopo hiyo huku serikali ikiwasisitiza wanafunzi hao kutumia mikopo hiyo kwa lengo lililokusudiwa.
Share:

0 comments:

Post a Comment

YouTube

Blog Archive

Pages

Our Facebook Page

Hali ya Hewa

Waliotembelea