Wednesday 19 October 2016

Waziri Mkuu aagiza wanaoharibu mazingira kuchukuliwa hatua


Waziri Mkuu KASSIM MAJALIWA ameuagiza uongozi wa mkoa wa LINDI kuhakikisha wanawakamata na kuwachukulia hatua za kisheria
Waziri Mkuu KASSIM MAJALIWA ameuagiza uongozi wa mkoa wa LINDI kuhakikisha wanawakamata na kuwachukulia hatua za kisheria watu wote wanaoharibu mazingira kwa kufyeka na kuchoma moto misitu. 
Waziri Mkuu MAJALIWA ametoa agizo hilo kwa nyakati tofauti wakati akizungumza na wananchi wa wilaya ya RUANGWA kwenye mikutano ya hadhara ambapo amesema mkoa huo uko hatarini kugeuka jangwa na tayari vyanzo vingi vya maji vimeanza kukauka kwa sababu ya uharibifu wa mazingira unaosababisha ukame.
Kwa upande wake Mkuu wa Mkoa wa LINDI, GODFREY ZAMBI, amewataka watendaji wa kata na vijiji kuimarisha ulinzi wa maeneo ya misitu na maji na atakayeshindwa atachukuliwa hatua kali za kisheria.
Wakati huo huo Mke wa Waziri Mkuu MARY MAJALIWA
ameiomba jamii ya watanzania kuwasaidia watoto wenye ulemavu wa ngozi.
Mama MAJALIWA ameyasema hayo wakati alipokwenda kutoa misaada kwa watoto wenye ulemavu huo katika kijiji cha MITOPE kilichopo wilaya ya RUANGWA Mkoani LINDI.
Share:

0 comments:

Post a Comment

YouTube

Blog Archive

Pages

Our Facebook Page

Hali ya Hewa

Waliotembelea